🦜 Taifa Leo
@taifaleo.nation.co.ke@rss-parrot.net
I'm an automated parrot! I relay a website's RSS feed to the Fediverse. Every time a new post appears in the feed, I toot about it. Follow me to get all new posts in your Mastodon timeline!
Brought to you by the RSS Parrot.
---
Your feed and you don't want it here? Just
e-mail the birb.
Wito serikali iimarishe sera ya kutetea haki za wajane nchini
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/wito-serikali-iimarishe-sera-ya-kutetea-haki-za-wajane-nchini/
Published: March 25, 2026 15:50
BAADA ya kifo cha mumewe mwaka wa 2008, maisha ya Josephine Wainaina yalibadilika ghafla.
Akiwa na umri wa miaka 53 sasa, anakumbuka kwa uchungu jinsi alivyohangaika pamoja na watoto wake wawili.
“Nilipoteza kila kitu. Tulitoka pale tulipokuwa tunaishi…
Vijana wataka mageuzi katika uongozi wa jiji la Nairobi
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/vijana-wataka-mageuzi-katika-uongozi-wa-jiji-la-nairobi/
Published: March 25, 2026 14:53
VIJANA katika eneo la Riruta Satellite jijini Nairobi wameeleza hitaji la dharura la kubadilishwa kwa mfumo wa uongozi wa jiji ili kukabiliana na changamoto sugu zinazowakumba wakazi.
Haya yaliibuka wakati wa kongamano la kwanza la kushirikisha umma…
Hizi hapa sababu mifereji ya ufadhili ya Umoja wa Mataifa haipaswi kukauka
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/hizi-hapa-sababu-mifereji-ya-ufadhili-ya-umoja-wa-mataifa-haipaswi-kukauka/
Published: March 25, 2026 13:16
MAPEMA Januari mwaka huu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Antonio Guterres alitoa ujumbe wa kuatua moyo kwa nchi wanachama wa UN.
Alionya kuhusu hali tete katika asasi hiyo ya kimataifa huku akiongeza kuwa shirika hilo lilikuwa katika hatari ya…
TAHARIRI: Vijana wasikubali ‘Niko Kadi’ itekwe na wanasiasa
https://taifaleo.nation.co.ke/tahariri/tahariri-vijana-wasikubali-niko-kadi-itekwe-na-wanasiasa/
Published: March 25, 2026 12:12
GEN Z wanastahili kujihadhari kaulimbiu yao ya ‘Niko Kadi’ isitekwe nyara na wanasiasa wanaolenga kuitumia kujivumisha wakisaka uongozi mwaka ujao.
Niko Kadi imekuwa kauli maarufu ambayo vijana wanatumia kuhimizana wajitokeze kujisajili kama wapigakura kwa…
Kioja mtaani baada ya msupa kupatikana na mizoga ya paka
https://taifaleo.nation.co.ke/dondoo/kioja-mtaani-baada-ya-msupa-kupatikana-na-mizoga-ya-paka/
Published: March 25, 2026 11:49
MASII, MACHAKOS
MWANADADA mmoja katika mtaa huu amegeuka gumzo miongoni mwa majirani baada ya kudaiwa kupatikana na vitu vya kutatanisha vinavyohusishwa na uchawi.
Kisa kilianza mizoga kadhaa ya paka ilipopatikana karibu na njia ya kuelekea kwake katika…
Kombe la Dunia: Bei ya tiketi yazua kilio
https://taifaleo.nation.co.ke/dimba/kombe-la-dunia-bei-ya-tiketi-yazua-kilio/
Published: March 25, 2026 10:22
LONODN, UINGEREZA
Chama cha Mashabiki wa Soka barani Ulaya (FSE) kimewasilisha malalamishi rasmi dhidi ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kikilalamikia “bei ghali zaidi za tiketi” za Kombe la Dunia la mwaka huu.
FSE, kwa ushirikiano na…
Vijana Afrika wataka mifumo jumuishi ya chakula kufungua ajira na ubunifu
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/vijana-afrika-wataka-mifumo-jumuishi-ya-chakula-kufungua-ajira-na-ubunifu/
Published: March 25, 2026 07:59
VIJANA barani Afrika wanaendelea kushinikiza ajenda ya mifumo jumuishi ya chakula ili kufungua nafasi za ajira na ubunifu kwenye mtandao wa uchakataji mazao ya kilimo, wakitaka sekta hiyo kutambuliwa upya kama chanzo cha biashara na mabadiliko ya uchumi.…
Nyasi ya ‘juncao’ inayokomaa upesi yaibuka kimbilio kwa wenye mifugo
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/akili-mali/nyasi-ya-juncao-inayokomaa-upesi-yaibuka-kimbilio-kwa-wenye-mifugo/
Published: March 25, 2026 07:55
WAKULIMA nchini wamelazimika kubadili mbinu zao za kilimo na kukumbatia teknolojia zinazostahimili athari za mabadiliko ya tabianchi, kuanzia ukame wa muda mrefu, mafuriko hadi wadudu na magonjwa yanayoharibu mazao.
Kwa Abdirahman Ali Hassan, mfugaji…
Msitumie vifo vya binti zetu kujikweza kisiasa, familia zaonya
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/msitumie-vifo-vya-binti-zetu-kujikweza-kisiasa-familia-zaonya/
Published: March 25, 2026 06:55
FAMILIA mbili katika kaunti za Nyeri na Murang’a zimewataka wanasiasa kuacha kutumia majina ya wapendwa wao waliofariki katika mijadala ya kisiasa iliyoenea katika mikutano ya hadhara wiki mbili zilizopita.
Familia za Regina Wairimu na Maureen Kinyua…
Asilimia 87 ya Wakenya wanatatizika kifedha na kiakili, utafiti waonyesha
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/afya-na-jamii/asilimia-87-ya-wakenya-wanatatizika-kifedha-na-kiakili-utafiti-waonyesha/
Published: March 25, 2026 05:55
KWA muda wa miezi tisa, Emily (si jina lake halisi) aliendelea kwenda kazini akitumaini mwajiri wake angemlipa mshahara wake mwisho wa mwezi.
Lakini siku ya malipo ilipowadia, hakupokea taarifa yoyote kutoka benki.
Mwajiri wake aliendelea kutoa ahadi…
Utafutaji mahari ndio unachangia wizi wa mifugo, Waziri Murkomen asema
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/utafutaji-mahari-ndio-unachangia-ongezeko-la-wizi-wa-mifugo-waziri-asema/
Published: March 25, 2026 04:55
WIMBI la ujangili na wizi wa mifugo lililosababisha vifo vya watu wengi na kuibwa kwa maelfu ya mifugo linachochewa na shinikizo za kitamaduni kwa vijana wanaotaka kuoa.
Waziri wa Usalama wa Ndani, Bw Kipchumba Murkomen, alisema visa vya wizi wa mifugo…
Ushirikiano wa Kenya na Somalia wasifiwa kupunguza ugaidi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/ushirikiano-wa-kenya-na-somalia-wasifiwa-kupunguza-ugaidi/
Published: March 25, 2026 03:55
USHIRIKIANO uliopo kati ya Jeshi la Kenya (KDF), vitengo mbalimbali vya polisi, walinda usalama wa nchi jirani ya Somalia na jamii umetajwa kufaulisha pakubwa vita dhidi ya Al-Shabaab katika Kaunti ya Lamu na maeneo ya mpakani mwa Kenya na Somalia.…
Hofu upungufu wa mafuta ukiripotiwa Kenya
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/hofu-upungufu-wa-mafuta-ukiripotiwa-kenya/
Published: March 25, 2026 02:55
KAULI ya Waziri wa Kawi na Petroli Opiyo Wandayi, kwamba Kenya ina akiba ya kutosha ya mafuta imeendelea kuzua utata, huku hali halisi ikionyesha vituo vingi vya mafuta kote nchini vimeanza kukosa bidhaa hiyo muhimu.
Bw Wandayi alijaribu kutuliza hofu ya…
Iran: Kauli ya Trump kuhusu muafaka ni feki
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/iran-kauli-ya-trump-kuhusu-muafaka-ni-feki/
Published: March 24, 2026 12:52
TEHRAN, Iran
IRAN Jumanne iliendelea kuirushia Israeli makombora licha ya Rais Donald Trump kusema kuwa wameanza mazungumzo ya kusitisha vita Ukanda wa Mashariki ya Kati.
Israeli ilithibitisha kuwa ilishambuliwa ilhali Trump, Rais wa Amerika, alikuwa…
Amebobea kuchoma nyama kwa kutumia moshi
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/amebobea-kuchoma-nyama-kwa-kutumia-moshi/
Published: March 24, 2026 12:31
KILICHOANZA kama burudani ya kupikia familia na marafiki nyumbani karibu miaka kumi iliyopita kwa Steve Gitu, sasa kimegeuka kuwa fursa kubwa ya kibiashara.
Leo hii, Gitu ni mwanzilishi wa Rib Racks Ltd, kampuni inayojihusisha na uchomaji wa nyama na…
Jombi ahamisha makazi ufukweni ili kuhepa kero za mke nyumbani
https://taifaleo.nation.co.ke/dondoo/jombi-ahamisha-makazi-ufukweni-ili-kuhepa-kero-za-mke-nyumbani/
Published: March 24, 2026 12:04
AMU KISIWANI, LAMU
JOMBI mmoja kisiwani Lamu amewaacha wengi vinywa wazi baada ya kuamua kuhamisha makazi yake hadi karibu na bahari, akisema huko ndiko amepata utulivu wa kweli.
Jamaa huyo amejitengenezea maskani ndogo karibu na ufukwe wa Bahari Hindi…
Jinsi hifadhi za kijamii zinavyoendeleza biashara licha ya kusitishwa kwa ufadhili wa USAID
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/jinsi-hifadhi-za-kijamii-zinavyoendeleza-biashara-licha-ya-kusitishwa-kwa-ufadhili-wa-usaid/
Published: March 24, 2026 11:16
HIFADHI nyingi za wanyamapori za kijamii Kenya zimekuwa zikitegemea kwa kiasi kikubwa ufadhili wa wahisani kutoka nje ya nchi kuendesha shughuli, na kufuatia kusitishwa kwa ufadhili kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Amerika (USAID), sasa…
Mjane wa Ng’eno asalimu amri, ajiondoa kinyang’anyiro cha Emurua Dikirr
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/mjane-wa-ngeno-asalimu-amri-ajiondoa-kinyanganyiro-cha-emurua-dikirr/
Published: March 24, 2026 07:55
KAMPENI za kuwania mchujo wa UDA katika eneobunge la Emurua Dikirr zimefikia kipindi cha lala salama huku ikibainika wazi kuwa mjane wa marehemu mbunge Johana Ng’eno, amejiondoa kinyang’anyironi.
Naiyanoi Ng’eno alijiondoa kwenye mapambano ya kisiasa ya…
Kindiki ataka Sh450m zaidi za helikopta na chakula afisini mwake
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kindiki-ataka-sh450m-zaidi-za-helikopta-na-chakula-afisini-mwake/
Published: March 24, 2026 06:55
AFISI ya Naibu Rais Profesa Kithure Kindiki inataka Sh450 milioni kulipia shughuli za kila siku za afisi yake pamoja na kukodisha helikopta kulingana na stakabadhi kabla ya Bunge la Kitaifa.
Afisi ya Profesa Kindiki awali ilikuwa imetengewa Sh523 milioni…
Mkataba kutambua ODM na UDA kama washirika sawa, Wanga afichua
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/mkataba-kutambua-odm-na-uda-kama-washirika-sawa-wanga-afichua/
Published: March 24, 2026 05:55
MWENYEKITI wa ODM Gladys Wanga amesema kuwa ODM itajadiliana na UDA kama mshirika sawa na watamakinikia kutoingiliwa kwa ngome zao za kisiasa katika uchaguzi mkuu wa 2027.
Bi Wanga alisema muafaka kati yao na UDA utakuwa wa kina na utaangazia sera,…
Mashaka zaidi kwa Tuju polisi wakimshutumu kwa madai ya ‘kujiteka nyara’
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/mashaka-zaidi-kwa-tuju-polisi-wakimtia-mbaroni-kwa-madai-ya-kujiteka-nyara/
Published: March 24, 2026 04:55
MASHAKA zaidi yalijiri jana baada ya Waziri wa zamani wa Utalii, Raphael Tuju ambaye alikuwa ametoweka kwa siku mbili, kujitokeza katika makazi yake mtaa wa Karen, Nairobi.
Bw Tuju alijitokeza hadharani jana baada ya kuripotiwa kutoweka mnamo Jumamosi…
Makateli watishia kukwamisha mpango wa Ruto wa mbolea ya bei nafuu
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/makateli-watishia-kukwamisha-mpango-wa-ruto-wa-mbolea-ya-bei-nafuu/
Published: March 24, 2026 03:55
MPANGO maalum wa Rais William Ruto unaohusu kuboresha uzalishaji wa kilimo kupitia mbolea ya bei nafuu upo hatarini huku mashirika ya mabwanyenye yakiingilia na kuwatenga waliokusudiwa kunufaika kwayo.
Mtandao huo unaoendeshwa nchini kote, umekuwa…
Hofu familia zilizovutiwa na vyakula wakati wa Ramadhani zikikosa kurejea makwao
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/hofu-familia-zilizovutiwa-na-vyakula-wakati-wa-ramadhani-zikikosa-kurejea-makwao/
Published: March 24, 2026 02:55
WAKATI Waislamu walipohitimisha mwezi wao mtukufu wa Ramadhani Ijumaa iliyopita, changamoto ya kipekee imeibuka.
Katika kipindi chote cha Ramadhani, viongozi wengi wa kisiasa, mashirika ya kibiashara na wananchi wa kawaida walijihusisha na shughuli za…
Mafuriko yafanya demu amfokee mumewe kwa kutojenga ushago
https://taifaleo.nation.co.ke/dondoo/mafuriko-yafanya-demu-amfokee-mumewe-kwa-kutojenga-ushago/
Published: March 23, 2026 16:16
TENA, NAIROBI
MVUA kubwa inayoendelea kunyesha jijini Nairobi wiki iliyopita ilisababisha mzozo mkali kati ya mke na mume baada ya mwanamke huyo kumtaka mumewe amjengee nyumba ya mawe mashambani.
Mama huyo wa watoto wanne alimlaumu mumewe kwa kuchelewa…
Ushuhuda wa mtoto watumiwa kumfunga mshukiwa wa unajisi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/ushuhuda-wa-mtoto-watumiwa-kumfunga-mshukiwa-wa-unajisi/
Published: March 23, 2026 14:31
UAMUZI wa Mahakama Kuu mjini Malindi umemulika sheria kuhusu uzito wa ushahidi wa watoto katika kesi za makosa ya kingono, wakati ushahidi mwingine hauridhishi.
Hali hii ilijitokeza wakati mahakama ilipokuwa ikipitia hukumu ya kifungo cha miaka 30…
Kenya inavyoteka masoko ya kimataifa kupitia uzalishaji wa aina mpya ya maua
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/kenya-inavyoteka-masoko-ya-kimataifa-kupitia-uzalishaji-wa-aina-mpya-ya-maua/
Published: March 23, 2026 12:23
IKIWA imeorodheshwa kama nchi ya nne bora duniani katika uuzaji nje wa maua yaliyokatwa na ya mapambo, Kenya inaendelea kukumbatia aina mpya ya maua hatua inayoipanulia zaidi masoko ya kimataifa.
Kulingana na Afisa Mkuu Mtendaji wa Baraza la Maua Kenya…
Trump asitisha ghafla vita Iran saa chache kabla ya makataa ya kulipua vituo vya kawi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/trump-asitisha-ghafla-vita-iran-saa-chache-kabla-ya-makataa-ya-kulipua-vituo-vya-kawi/
Published: March 23, 2026 12:04
TEL AVIV/JERUSALEM/WASHINGTON,
RAIS Donald Trump amesitisha ghafla vita Iran, saa chache kabla ya muda wa saa 48 aliokuwa ameambia Iran ifungue Mkondo wa Hormuz lau sivyo alipue vituo vyote vya kawi nchini humo na kutumbukiza taifa nzima kwenye giza…
Utata wa miili ya Nyamira kuzikwa Kericho
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/utata-wa-miili-ya-nyamira-kuzikwa-kericho/
Published: March 23, 2026 11:08
UTATA umezuka kuhusu miili 14 ambayo ilizikwa kisiri katika Kaunti ya Kericho huku wamiliki wa makaburi, maafisa wa utawala wa kieneo, polisi na serikali ya kaunti hiyo wakionekana kutokuwa na ufahamu wowote kuhusu tukio hilo.
Maswali yameibuka kuhusu…
LUGHA: Makosa ya kukanusha sentensi bila kuzingatia viambishi vya ngeli husika
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/lugha-fasihi-elimu/lugha-makosa-ya-kukanusha-sentensi-bila-kuzingatia-viambishi-vya-ngeli-husika/
Published: March 23, 2026 07:55
UTUNGAJI wa sentensi sahihi za Kiswahili huzingatia ngeli. Ngeli ni kundi la nomino zenye sifa sawa kiupatanishi kisarufi.
Hata ingawa wapo wanafunzi wengi wanaoweza kutunga sentensi sahihi wakizingatia viambishi sahihi vya upatanisho wa kisarufi, wapo…
Miradi ya Ruto Nyanza ikikamilika kabla ya 2027 Upinzani mashakani -Wadadisi
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/jamvi-la-siasa/miradi-ya-ruto-nyanza-ikikamilika-kabla-ya-2027-upinzani-mashakani-wadadisi/
Published: March 23, 2026 06:55
ZIARA ya siku tano ya Rais William Ruto na ile ya siku nne Luo Nyanza iliyojaa miradi huenda imesambaratisha juhudi za Upinzani na Linda Mwananchi kupata uungwaji mkono eneo hilo kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.
Kwa miaka kadhaa, maeneo ya Nyanza na…
Maswali huku Tuju akitoweka zogo la mali yake likizidi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/maswali-huku-tuju-akitoweka-zogo-la-mali-yake-likizidi/
Published: March 23, 2026 05:55
WAZIRI wa zamani na ambaye pia alihudumu kama Katibu Mkuu wa Chama cha Jubilee anayekabiliwa na kipindi kigumu kuhusu mali yake, Raphael Tuju jana iliripotiwa kutoweka.
Wakili wake Paul Nyamodi alithibitisha kuwa Bw Tuju na dereva wake Steve Mwanga,…
Gen Z waibuka na ‘Niko Kadi’ wanayosema wataitumia kubadilisha uongozi 2027
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/gen-z-waibuka-na-niko-kadi-wanayosema-wataitumia-kubadilisha-uongozi/
Published: March 23, 2026 03:55
GEN -Z sasa wamerejea na wito wa ‘Niko Kadi’, kauli-mbiu ambayo wanalenga kuitumia kuwahimiza vijana wajisali kuwa wapigakura nchini kuanzia wiki ijayo ili kubadilisha uongozi wa nchi.
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imetangaza kuwa kutakuwa na…
Viongozi wa ODM Pwani wasisitiza ‘pawa si pawa bila Joho’
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/viongozi-wa-odm-pwani-wasisitiza-pawa-si-pawa-bila-joho/
Published: March 23, 2026 03:55
VIONGOZI wa kisiasa kutoka eneo la Pwani wameongeza wito wa kutaka uwakilishi mkubwa zaidi katika ngazi za juu za serikali, wakisisitiza kwamba Waziri wa Madini Hassan Joho awe mgombea mwenza wa Rais William Ruto katika uchaguzi wa 2027.
Wakizungumza…
Kalonzo na Wamalwa wadai kuna njama ya kumtia pingu Gachagua
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/kalonzo-na-wamalwa-wadai-kuna-njama-ya-kumtia-pingu-gachagua/
Published: March 23, 2026 03:25
VIONGOZI wa upinzani jana walidai kuwa kuna mpango wa kumkamata aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua na kumfikisha kortini.
Wakiongea katika Kaunti ya Murang’a jana, wanasiasa wa muungano wa upinzani walidai Bw Gachagua analengwa ili kuzima siasa zake…
Trump aapa kutumia mabavu Democrats wakizidi kumkazia
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/trump-aapa-kutumia-mabavu-democrats-wakizidi-kumkazia/
Published: March 23, 2026 02:55
WASHINGTON, AMERIKA
RAIS Donald Trump ametishia kutuma maajenti wa Idara ya Uhamiaji na Ushuru wa Bidhaa (ICE) kwenye viwanja vya ndege nchini, hii leo iwapo wabunge wa Democrat hawatakubali papo hapo ufadhili wa usalama wa uwanja wa ndege.
“Nitawahamisha…
Matumaini ya Arsenal kushinda ‘quadruple’ yayeyuka baada ya kipigo cha Man City
https://taifaleo.nation.co.ke/dimba/matumaini-ya-arsenal-kushinda-quadruple-yayeyuka-baada-ya-kipigo-cha-man-city/
Published: March 22, 2026 19:59
MATUMAINI ya miamba wa soka Arsenal kushinda mataji manne msimu huu yaliyeyushwa kwa njia aina yake pale Manchester City ilipowatandika 2-0 kwenye fainali ya Carabao Cup, ugani Wembley.
Vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza Arsenal walifungwa mabao hayo katika…
Wakenya kulipa Sh3bn kwa ziara za Ruto nje ya nchi kutoka sasa hadi Juni 30
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/wakenya-kulipa-sh3bn-kwa-ziara-za-ruto-nje-ya-nchi-kutoka-sasa-hadi-juni-30/
Published: March 22, 2026 15:40
WALIPA Ushuru wanatarajiwa kutoa Sh3.1 bilioni kufadhili ziara za Rais William Ruto nje ya nchi, ikiwa imesalia miezi miwili pekee kabla ya kutamatika kwa mwaka huu wa kifedha.
Stakabadhi ambazo zimewasilishwa bungeni zinaonyesha kuwa Wizara ya Masuala ya…
Kitendawili cha mbolea kukosekana msimu wa upanzi ukianza
https://taifaleo.nation.co.ke/habari-mseto/kitendawili-cha-mbolea-kukosekana-msimu-wa-upanzi-ukianza/
Published: March 22, 2026 14:37
SERIKALI inakabiliwa na kitendawili kigumu kusawazisha kati ya kuongeza uzalishaji wa mimea na kuwepo chakula cha kutosha kutokana na upungufu wa mbolea ya bei nafuu.
Hii ni licha ya mipango ya kununua kutoka nchi za kigeni mifuko 12.5 milioni ya kilogramu…
Tamko la Kindiki lamtosa kwenye tope aliloogelea mdosi wake
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/jamvi-la-siasa/tamko-la-kindiki-lamtosa-kwenye-tope-aliloogelea-mdosi-wake/
Published: March 22, 2026 11:53
NAIBU Rais Kithure Kindiki amedhihirisha uaminifu wake wa dhati kwa Rais William Ruto akimuunga kwa kuwarushia cheche kali wapinzani wake wa kisiasa kwa kumkosoa.
Akizungumza Jumatano, Machi 18, 2026, akiwa katika Kaunti ya Bomet, Kindiki aliwashutumu…
Wakazi wapata afueni Bomba la maji likikarabatiwa
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kaunti/wakazi-wapata-afueni-bomba-la-maji-likikarabatiwa/
Published: March 22, 2026 11:03
Ulimwengu unavyoadhimisha Siku ya Maji Dunian, makumi ya wanawake katika maeneo ya ukame ya Kaunti ndogo ya Kajiado West walipata afueni baada ya ukarabati wa bomba kubwa la maji ambalo lilikuwa limeharibika na kutotumika kwa miaka 15.
Kwa zaidi ya muongo…
Uhaba wa mafuta washuhudiwa nchini licha ya serikali kusisitiza kuna akiba ya kutosha
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/uhaba-wa-mafuta-washuhudiwa-nchini-licha-ya-serikali-kusisitiza-kuna-akiba-ya-kutosha/
Published: March 22, 2026 10:49
UHABA wa mafuta umeanza kushuhudiwa katika maeneo mbalimbali nchini huku madereva wakiripoti kuyakosa vituoni, licha ya serikali kusisitiza akiba ya kitaifa bado iko thabiti.
Katika jiji la Nairobi, hasa kwenye Barabara ya Lang’ata, baadhi ya vituo vya…
Rais Ruto anatarajiwa kupeleka minofu Nyanza baada ya ziara yake ya Magharibi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/rais-ruto-anatarajiwa-kupeleka-minofu-nyanza-baada-ya-ziara-yake-ya-magharibi/
Published: March 21, 2026 07:55
BAADA ya kukamilisha ziara ya siku nne katika eneo la Magharibi, Rais William Ruto anatarajiwa kuanza mojawapo ya majukumu muhimu zaidi ya kisiasa ya kuwashawishi wakazi wa Nyanza kuunga mkono makubaliano ya kabla ya uchaguzi kati ya serikali yake na…
Wamuthende akosa kufika kortini kuhojiwa kuhusu kesi ya kupinga ushindi wake
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/wamuthende-akosa-kufika-kortini-kuhojiwa-kuhusu-kesi-ya-kupinga-ushindi-wake/
Published: March 21, 2026 06:55
KESI ya kupinga matokeo ya uchaguzi mdogo wa eneo la Mbeere North umechukua mkondo mpya baada ya Mbunge Leo Wamuthende Njeru kukosa kufika mbele ya mahakama kuhojiwa, akiamua kutegemea tu hati yake ya kiapo aliyowasilisha.
Hatua hiyo imeibua upinzani…
MAFURIKO: Mmoja afa mvua kubwa ikianza maeneo mengi kama ilivyotabiriwa
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/mafuriko-mmoja-afa-mvua-kubwa-ikianza-maeneo-mengi-kama-ilivyotabiriwa/
Published: March 21, 2026 05:55
MVUA kubwa ilianza kunyesha Nairobi na sehemu zingine za nchi Ijumaa alasiri, ilivyotabiriwa na Idara ya Hali ya Hewa.
Tofauti na Ijumaa nyingine, mitaa ya jiji ilikuwa wazi zaidi kutokana na likizo ya Idd-ul-Fitr, inayoadhimisha mwisho wa mwezi mtukufu…
Mataifa ya Mashariki ya Kati yaadhimisha Idd huku mapambano kati ya Iran, Amerika na Israeli yakichacha
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/mataifa-ya-mashariki-ya-kati-yaadhimisha-idd-huku-mapambano-kati-ya-iran-amerika-na-israeli-yakichacha/
Published: March 21, 2026 04:55
MATAIFA ya Mashariki ya Kati kama vile Saudia Arabia wanasherehekea sikukuu ya Idd mashambulizi yakiendelea kati ya Iran, Israeli na Amerika.
Sikukuu ya Idd katika Mataifa ya Ghuba zitafanyika katika misikiti ya kawaida badala ya umati wa watu kukusanyika…
Idd: Wito viongozi wakome matamshi ya chuki na matusi uchaguzi wa 2027 ukikaribia
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/idd-wito-viongozi-wakome-matamshi-ya-chuki-na-matusi-uchaguzi-wa-2027-ukikaribia/
Published: March 21, 2026 03:55
VIONGOZI wa Kiislamu wameungana na viongozi wengine wa kidini kote nchini kukemea matamshi ya ukosefu wa maadili miongoni mwa wanasiasa, wakionya kuwa malumbano ya sasa ya kisiasa yanaweza kuhatarisha umoja wa taifa huku nchi ikielekea Uchaguzi Mkuu wa…
ODM kuandaa NDC vita vya ubabe vikiendelea
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/odm-kuandaa-ndc-vita-vya-ubabe-vikiendelea/
Published: March 21, 2026 02:55
MIKUTANO ya wajumbe wa kitaifa ya vyama vya kisiasa nchini mara nyingi huwa mahali ambapo nyota za kisiasa huzaliwa huku nyingine zikizimika ghafla.
Katika historia ya siasa za Kenya, mikutano hii imekuwa na nguvu kubwa ya kuamua mustakabali wa vyama na…
Nyota wa filamu Chuck Norris amefariki dunia
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/nyota-wa-filamu-chuck-norris-amefariki-dunia/
Published: March 20, 2026 15:33
MUIGIZAJI mashuhuri wa filamu za mapigano na bingwa wa zamani wa karate, Chuck Norris, amefariki dunia, familia yake ilitangaza kupitia taarifa iliyochapishwa katika akaunti yake ya Instagram Ijumaa Machi 20, 2026.
Katika taarifa hiyo, familia yake…
Israeli yadai kumuua kiongozi mwingine wa ngazi ya juu wa Iran
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/israeli-yadai-kumuua-kiongozi-mwingine-wa-ngazi-ya-juu-wa-iran/
Published: March 20, 2026 13:59
SERIKALI ya Israeli imedai kuwa imemuua Waziri wa Ujasusi wa Iran, Esmail Khatib, katika mashambulizi yaliyofanywa usiku wa kuamkia Jumatano.
Haya yanajiri huku Tehran ikifanya misa ya pamoja ya kuwazika maafisa wake waliouliwa wakiwemo Ali Larijani…
Ufugaji nyuki kwa kutumia mbinu za kisasa unavyomuingizia mamilioni
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/ufugaji-nyuki-kwa-kutumia-mbinu-za-kisasa-unavyomuingizia-mamilioni/
Published: March 20, 2026 11:45
UZOEFU wa miaka 12 wa Joseph Karuga katika sekta ya kilimo na mifugo umemchochea kubadilisha tasnia ya ufugaji nyuki nchini Kenya, hatua ambayo sasa inamwingizia mamilioni ya pesa.
Awali, Karuga alifanya kazi katika sekta ya mazao na ufugaji nyuki kwenye…
Jinsi mhandisi alivyogeuka mkulima na kujenga himaya ya kanga na kuku
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/jinsi-mhandisi-alivyogeuka-mkulima-na-kujenga-himaya-ya-kanga-na-kuku/
Published: March 20, 2026 10:59
KILOMITA chache kutoka mji wa Kitengela, Kaunti ya Kajiado, mfugaji mmoja anaonekana kubadilisha taswira ya dhana ya eneo hilo linalojulikana kama kame (ASAL).
Kajiado, ni maarufu kwa ufugaji wa ng’ombe wa nyama ikizingatiwa kuwa kiwango chake kikubwa cha…
Ruto ahimiza Wakenya kudumisha umoja na upendo Waislamu wanaposherehekea Idd
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/ruto-ahimiza-wakenya-kudumisha-umoja-na-upendo-waislamu-wanaposherehekea-idd/
Published: March 20, 2026 09:57
RAIS William Ruto amewataka Wakenya kudumisha umoja na upendo wakati huu ambapo waumini wa Kiislamu wanaadhimisha siku kuu ya Idd ul-Fitr.
Kwenye taarifa aliyoitoa Machi 20, 2026 baada ya kukamilika kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadan kiongozi wa taifa aliwataka…
Ripoti yafichua madiwani wanatumia karibu bilioni kutalii dunia kaunti zikikosa pesa
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/ripoti-yafichua-madiwani-wanatumia-karibu-bilioni-kutalii-dunia-kaunti-zikikosa-pesa/
Published: March 20, 2026 07:55
KAUNTI 41 nchini zilitumia jumla ya Sh822 milioni kwa safari za nje ya nchi ndani ya kipindi cha miezi sita, licha ya hatua za kubana matumizi zilizotangazwa na Rais William Ruto miaka miwili iliyopita.
Ripoti mpya ya Mdhibiti wa Bajeti Margaret Nyakang’o…
Askari-gongo mashakani mbunge akipendekeza kazi zao zifanywe na waliofuzu NYS
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/askari-gongo-mashakani-mbunge-akipendekeza-kazi-zao-zifanywe-na-nys/
Published: March 20, 2026 06:55
WALINZI wa kibinafsi nchini huenda wakakabiliwa na ushindani mkali au hata kupoteza ajira katika baadhi ya taasisi za umma na kibinafsi iwapo Bunge litapitisha hoja inayopendekeza wanaohitimu kutoka Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS) watwae kazi hizo.
Hoja…
Kindiki ashuhudia mvutano kuhusu kiti chake Pwani
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/kindiki-ashuhudia-mvutano-kuhusu-kiti-chake-pwani/
Published: March 20, 2026 05:55
NAIBU Rais Kithure Kindiki alirudi katika eneo la Pwani na kukutana na mvutano wa kisiasa kati ya wanasiasa wa chama tawala cha United Democratic Alliance (UDA) na kile cha Orange Democratic Movement (ODM) wanaomenyania nafasi yake wakati wa uchaguzi ujao.…
Mnajiaibisha kwa kutukanana, maaskofu wakemea viongozi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/mnajiaibisha-kwa-kutukanana-maaskofu-wakemea-viongozi/
Published: March 20, 2026 04:55
MAASKOFU wa Kanisa Katoliki Kenya wamelaani vikali matusi yanayoendelea kati ya Rais William Ruto na viongozi wa upinzani, wakitaka wanasiasa kupunguza maneno makali katika majukwaa ya umma.
Akizungumza jana, mwenyekiti wa Baraza Kuu la Maaskofu hao…
Gachagua amjibu Ruto, aibua madai mapya ya ufisadi
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/gachagua-amjibu-ruto-aibua-madai-mapya-ya-ufisadi/
Published: March 20, 2026 03:55
ALIYEKUWA Naibu Rais Rigathi Gachagua amemjibu vikali Rais William Ruto, akimlaumu kwa “kudunisha hadhi ya urais” kwa kuzungumzia maisha ya kibinafsi ya watu badala ya masuala mazito yanayoikabili nchi.
Akizungumza katika makao makuu ya chama chake…
Ni furaha na mapochopocho Waislamu wakiadhimisha Idd baada ya kufunga
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/ni-furaha-na-mapochopocho-waislamu-wakiadhimisha-idd-baada-ya-kufunga/
Published: March 20, 2026 02:55
WAISLAMU kote nchini Kenya wanajiandaa kushuhudia rasmi mwandamo wa mwezi wa Shawwal, unaobainisha mwisho kamili wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Tayari, Waziri wa Usalama wa Ndani, Kipchumba Murkomen, ametangaza leo Ijumaa kuwa sikukuu kuadhimisha…
Iran: Hatutasusia kushiriki Kombe la Dunia ila hatukanyagi Amerika
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/iran-hatutasusia-kushiriki-kombe-la-dunia-ila-hatukanyagi-amerika/
Published: March 19, 2026 12:55
TIMU ya Taifa ya Iran imesema inaendelea na mipango ya kujiandaa kwa Kombe la Dunia na haina nia ya kujiondoa kwa kipute hicho hata kama hawataelekea Amerika.
Mkuu wa Shirikisho la Soka Iran Mehdi Taj alisema kuwa hawatajiondoa Kombe la Dunia ingawa…
Ukipata tiketi ya urais, nitakuunga mkono, Arati aambia Matiang’i
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kaunti/ukipata-tiketi-ya-urais-nitakuunga-mkono-arati-aambia-matiangi/
Published: March 19, 2026 11:18
Gavana wa Kisii Simba Arati amedokeza kuwa yuko tayari kumuunga mkono naibu kiongozi wa chama cha Jubilee Dkt Fred Matiang’i katika azma yake ya urais ila kwa sharti moja; ikiwa mrengo wa upinzani utamteua Waziri huyo wa zamani wa Usalama wa Ndani Dkt Fred…
Anwani ‘Nguu za Jadi’ ilivyo faafu kurejelea riwaya
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/lugha-fasihi-elimu/anwani-nguu-za-jadi-ilivyo-faafu-kurejelea-riwaya/
Published: March 19, 2026 10:45
ANWANI ya riwaya hii imeundwa kwa maneno mawili ambayo matumizi yake ni ya kijazanda.
Nguu ni vilele vya milima. Neno hili li metumika kijazanda kuashiria upeo wa juu wa mila au tam aduni kandamizi zilipofika hivyo kupuuzwa na kukiukwa na wanaodhulumiwa…
Sifa bainifu na jinsi ya kuandika Insha ya Tahakiki
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/lugha-fasihi-elimu/sifa-bainifu-na-jinsi-ya-kuandika-insha-ya-tahakiki/
Published: March 19, 2026 09:41
JUMA hili naomba tuangazie uandishi wa insha ya tahakiki. Tahakiki ni maandishi yanayoandikwa kwa nia ya kuchambua kazi fulani ya kisanii.
Tahakiki huandikwa baada ya kuisoma kazi hiyo na kuielewa vizuri.
Aghalabu vitabu vya fasihi andishi kama vile…
Alianzisha mradi wa mbuzi wa maziwa ambao ni bora zaidi nchini akiwa angali chuoni
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/alianzisha-mradi-wa-mbuzi-wa-maziwa-ambao-ni-bora-zaidi-nchini-akiwa-angali-chuoni/
Published: March 19, 2026 08:37
MAJAJI walipotembelea banda la maonyesho la Caleb Mwenda katika Maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo na Kibiashara ya Nairobi 2025 yaliyoandaliwa na Agricultural Society of Kenya (ASK) Jamhuri Grounds, Nairobi, mkulima huyo mchanga hakujua jitihada zake katika…
Mkakati wa Ruto kupanga viongozi wa Kenya Kwanza wafichuliwa
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/mkakati-wa-ruto-kupanga-viongozi-wa-kenya-kwanza-wafichuliwa/
Published: March 19, 2026 07:55
RAIS William Ruto anatekeleza mkakati unaochanganya mbinu za kisiasa na kiutawala ili kuleta vyama tanzu katika muungano wa Kenya Kwanza chini ya chake cha UDA.
Hatua hiyo inalenga kujiimarisha kisiasa na kuongeza nafasi ya kuchaguliwa tena katika Uchaguzi…
Utata wa Idd waibuka tena mfungo wa Ramadhani ukitamatika
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/utata-wa-idd-waibuka-tena-mfungo-wa-ramadhani-ukitamatika/
Published: March 19, 2026 06:55
HUKU mwezi mtukufu wa Ramadhani ukitamatika, tofauti za kuandama kwa mwezi zimejitokeza na kusababisha sikukuu ya Idd-ul-Fitr kusherehekewa siku tofauti miongoni mwa Waislamu.
Baadhi ya waumini hao wanasema Eid itakuwa leo Alhamisi huku wengine wakitaja…
Utaacha siasa za kumezea mate kiti cha Kindiki, Hassan Omar amuonya Joho
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/utaacha-siasa-za-kumezea-mate-kiti-cha-kindiki-hassan-omar-amuonya-joho/
Published: March 19, 2026 05:55
SIKU chache tu baada ya Rais William Ruto na Kinara wa ODM Bw Oburu Odinga kutoa wito wa kukomeshwa kwa uhasama wa kisiasa kati ya viongozi wa vyama vya ODM na UDA eneo la Pwani, Katibu Mkuu wa chama tawala Bw Hassan Omar, amejitokeza na kuanza kumshtumu…
Trump aambia Nato wamefanya ‘kosa la kijinga’ kukataa kumsaidia vitani Iran
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/trump-aambia-nato-wamefanya-kosa-la-kijinga-kukataa-kumsaidia-vitani-iran/
Published: March 19, 2026 04:55
WASHINGTON, AMERIKA
RAIS wa Amerika, Donald Trump amesema kuwa nchi yake ilifahamishwa na washirika wake wengi katika Muungano wa NATO kuwa hawataki kuingilia vita dhidi ya Iran, akisema hatua hiyo ni ‘kosa la kijinga’.
Trump alionekana kukerwa na hatua…
Winnie Odinga ang’ang’ania na makundi pinzani ya Oburu na Sifuna
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/winnie-odinga-angangania-na-makundi-pinzani-ya-oburu-na-sifuna/
Published: March 19, 2026 03:55
MBUNGE wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Winnie Odinga anaonekana kung'ang'aniwa na mirengo miwili ndani ya ODM kufuatia pendekezo awe naibu kiongozi wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) chini ya mjomba wake Dkt Oburu Oginga.
Ndani ya mrengo…
Jinsi ‘YouTube’ ilimpa wazo la ufugaji nyuki na kumgeuza mfanyabiashara hodari
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/akili-mali/jinsi-youtube-ilimpa-wazo-la-ufugaji-nyuki-na-kumgeuza-mfanyabiashara-hodari/
Published: March 18, 2026 07:55
KIJIJI cha Bobaracho, eneobunge la Nyaribari Chache, Kaunti ya Kisii kina mradi mzuri wa ufugaji nyuki.
Mradi huo unamilikiwa na Peter Mautia, 24, ambaye aliuanzisha baada ya kutazama video moja kwenye mtandao wa YouTube.
Jarida la Akilimali lilipata fursa…
Jiandaeni kwa gharika nyingine Alhamisi, Idara ya Utabiri yaonya Wakenya
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/jiandaeni-kwa-gharika-nyingine-alhamisi-idara-ya-utabiri-yaonya-wakenya/
Published: March 18, 2026 06:55
IDARA ya Utabiri wa Hali ya Hewa nchini Kenya imeonya kuwa mvua itaongezeka kuanzia Alhamisi, Machi 19, 2026, katika maeneo kadhaa ya nchi huku msimu wa mvua ndefu ukianza kushika kasi.
Katika utabiri wake wa hali ya hewa wa kila wiki wa Machi 17 hadi…
Mbinu nafuu ya kiasili inayosaidia katika utunzaji wa vifaranga
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/akili-mali/aelezea-mbinu-nafuu-inayosaidia-katika-utunzaji-wa-vifaranga/
Published: March 18, 2026 05:55
ENEO la Tuigoin katika Kaunti ya Trans-Nzoia, linafahamika kwa hali nzuri ya hewa inayochangia ukuzaji wa aina mbalimbali ya vyakula na ufugaji wa wanyama.
Pauline Sambu, ni mmoja wa wakazi wa eneo hilo. Yeye huuza vifaranga.
Tunapomtembelea, anafunguka…
Wakenya wasimulia masaibu ya kutiliwa ‘mchele’ wakiwa Safari Rally
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/wakenya-wasimulia-masaibu-ya-kutiliwa-mchele-wakiwa-safari-rally/
Published: March 18, 2026 04:55
VISA kadhaa vimeibuka kuhusu watu kuwekewa dawa kwenye vinywaji na kupoteza pesa katika Mashindano ya Safari Rally (WRC) yaliyofanyika Naivasha wikendi.
Mashindano hayo ya siku tatu yanayofanyika kila mwaka ambayo ni sehemu ya tamasha mashuhuri ya 2026,…
Wanafunzi waliochagua STEM Gredi 10 wakosa walimu waliohitimu kuwafundisha
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/wanafunzi-waliochagua-stem-gredi-10-wakosa-walimu-waliohitimu-kuwafundisha/
Published: March 18, 2026 04:25
WANAFUNZI wa Gredi 10 waliochagua masomo ya kiufundi katika shule za sekondari ya juu chini ya mkondo wa sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati (STEM) wamekaa bila kufundishwa tangu Januari kutokana na ukosefu wa walimu waliosomea taaluma hizo.
Huku…
Ruto, Upinzani waweka ustaarabu kando na kunyesheana makombora ya kudhalilisha
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kitaifa/ruto-upinzani-waweka-ustaarabu-kando-na-kunyesheana-makombora-ya-kudhalilisha/
Published: March 18, 2026 03:55
RAIS William Ruto jana alitumia ziara yake Magharibi mwa Kenya kushambulia vikali viongozi wa upinzani na kufungua malumbano makali ya kisiasa.
Kilichoanza kama ziara ya maendeleo kilibadilika haraka baada ya rais kuvua nembo ya kiongozi wa kitaifa…
Damu ni nzito: Winnie atangaza yuko tayari kushirikiana na kundi la Oburu
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/damu-ni-nzito-winnie-atangaza-yuko-tayari-kushirikiana-na-kundi-la-oburu/
Published: March 18, 2026 02:55
MBUNGE wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) Winnie Odinga, ametangaza kuwa yuko tayari kushirikiana na mrengo wa amu yake Oburu Oginga, ili kuimarisha chama cha Orange Democratic Movement (ODM) nchini.
Hapo awali, mbunge huyo alikuwa akihusishwa na kundi la…
Viongozi wanajivua busara kwa kurushiana matusi
https://taifaleo.nation.co.ke/maoni/viongozi-wanajivua-busara-kwa-kurushiana-matusi/
Published: March 17, 2026 18:02
Malumbano makali ya kisiasa yanayoendelea kati ya Rais William Ruto na baadhi ya vinara wa upinzani yameanza kuzua wasiwasi miongoni mwa wananchi kuhusu heshima na hadhi ya uongozi nchini.
Kauli za cheche zinazotupiana pande hizi mbili zinaonekana kama…
PAA yapaa na kutua kwa Wilbaro
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kaunti/paa-yapaa-na-kutua-kwa-wilbaro/
Published: March 17, 2026 17:02
HATIMAYE chama cha Pamoja African Alliance kimeamua kujiunga na kile cha Rais William Ruto cha UDA na kutangaza rasmi kwamba hakitasimamisha mgombea yeyote kwenye uchaguzi mkuu wa 2027.
Spika wa Bunge la Seneti Bw Amason Kingi, alitangaza kuwa chama hicho…
Israel yadai imemuua mkuu wa jeshi, Mojtaba akisema vita lazima viendelee
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/kimataifa/israel-yadai-imemuua-mkuu-wa-jeshi-mojtaba-akisema-vita-lazima-viendelee/
Published: March 17, 2026 12:48
JERUSALEM, ISRAEL
WAZIRI wa Ulinzi wa Israel Katz Jumanne, Machi 17, 2026 alidai kuwa wanajeshi wa Amerika-Israel walimuua mkuu wa jeshi la Iran na mkuu wa wapiganaji wa Basij kwenye misururu ya mashambulizi ya angani Jumatatu siku.
Iran nayo haiwaachi…
Wanavyoingiza mamilioni ya pesa kwa kubinafsisha asali kulingana na mahitaji ya soko
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/wanavyoingiza-mamilioni-ya-pesa-kwa-kubinafsisha-asali-kulingana-na-mahitaji-ya-soko/
Published: March 17, 2026 11:14
MWAKA 2021, Anthony Mwangi alimtembelea mshirika wake wa sasa wa kibiashara, Henry Guchu, na mkebe wa asali uliokuwa mezani ulichochea wazo la uwekezaji ambalo leo hii wanajivunia.
Wawili hawa ni wanafamilia, na Mwangi alikuwa amemtembelea shemeji yake…
SHAIRI: Lala pema Khamenei
https://taifaleo.nation.co.ke/mashairi/lala-pema-khamenei/
Published: March 17, 2026 11:03
Kwa jina lake Karima, Yarrabi Allah Manani,Natetema natetema, aloyafanza shetwani,Wa Marekani mnyama, na nguruwe mzayuni,Walovamia Irani, wakamuua mwandani.Unyama huo unyama, ukafiri ufatani,Walofanza zao njama, vigaro vya tini tini,Kwa Mola wana lawama,…
BI TAIFA – FAITH BITUTU
https://taifaleo.nation.co.ke/bi-taifa/bi-taifa-faith-bitutu/
Published: March 17, 2026 09:04
Anayetupambia ukurasa huu ni Bi Faith Bitutu, 22, ambaye ni mwanafunzi katika Chuo cha Rift Valley National Polytechnic. Uraibu wake ni kukutana na marafiki wapya na kusikiliza muziki, mapishi na kusoma. PICHA| RICHARD MAOSI
Wakulima Rift Valley wang’oa mahindi, majanichai na kukimbilia avokado
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/wakulima-rift-valley-wangoa-mahindi-majanichai-na-kukimbilia-avokado/
Published: March 17, 2026 07:55
WAKULIMA wanaomiliki mashamba madogomadogo katika kaunti kadhaa za Bonde la Ufa, wamegeukia kilimo cha parachichi almaarufu kama “dhahabu ya kijani kibichi” eneo hilo, baadhi waking’oa mazao yao ya mahindi na majanichai.
Soko la parachichi aina ya Hass…
Huzuni mama akirejea kutoka kazini na kupata bintiye ameuawa
https://taifaleo.nation.co.ke/habari/habari-za-kaunti/huzuni-mama-akirejea-kutoka-kazini-na-kupata-bintiye-ameuawa/
Published: March 17, 2026 06:55
KILICHOTARAJIWA kuwa wikendi ya kawaida kwa Glorious Kaiza mwenye umri wa miaka 11 kiligeuka kuwa janga baada ya mtoto huyo kutoweka Jumamosi, na baadaye mwili wake kupatikana mapema Jumapili asubuhi ukiwa umefungwa ndani ya mfuko katika eneo la Mjambere,…
Utata mwingine ODM makundi mawili yakipanga NDC sambamba
https://taifaleo.nation.co.ke/siasa/utata-mwingine-odm-makundi-mawili-yakipanga-ndc-sambamba/
Published: March 17, 2026 05:55
VITA vya kung’ang’ania mamlaka ndani ya ODM vimechukua mwelekeo mpya baada ya mrengo wa Linda Mwananchi kutangaza kuwa utakuwa na Kongamano sambamba wa Wajumbe (NDC) mnamo Machi 27.
Kinara wa ODM Dkt Oburu Oginga anatarajiwa kuongoza NDC siku hiyo huku…
Kaeni rada huku, mvua ndio imeshika kasi sasa, idara yaonya
https://taifaleo.nation.co.ke/makala/kaeni-rada-huku-mvua-ndio-imeshika-kasi-sasa-idara-yaonya/
Published: March 17, 2026 05:48
Idara ya Utabiri wa Hali ya Hewa nchini Kenya imeonya kuwa mvua itaongezeka kuanzia Alhamisi, Machi 19, 2026, katika maeneo kadhaa ya nchi huku msimu wa mvua ndefu ukianza kushika kasi.
Katika utabiri wake wa hali ya hewa wa kila wiki wa Machi 17 hadi…